AFISA MTENDAJI,
MAWAKALA WA PEMBEJEO KORTINI KWA RUSHWA
Na Bazil
Makungu Ludewa
TAASISI ya kuzuia na
kupambana na rushwa wilayani Ludewa katika Mkoa mpya wa Njombe imemfikisha
mahakamani kwa makosa kumi na tatu ya rushwa na udanganyifu Yohana Jenkin Pili
(50)afisa mtendaji wa kijiji cha Kipangala kilichopo katika kata ya Luilo
Ludewa.
Pamoja naye wengine
waliofikishwa katika mahakama hiyo ya hakimu mkazi Ludewa mjini ni pamoja na
Kilian Kilian Mbawala (40) mwenyekiti wa kamati ya pembejeo na Sebastian Haule(26)
mkazi wa Ludewa mjini ambaye ni wakala wa mbolea katika kijiji cha Kipangala.
Akisoma hati ya
mashtaka mbele ya Fredrick Lukuna hakimu mkazi katika mahakama ya wilaya
Ludewa, mwendesha mashtaka wa Takukuru Restituta Kesi aliiambia mahakama kuwa
washtakiwa wote kwa pamoja walitenda makosa hayo june mwaka huu.
Kesi akaongeza kuwa
Sebastian Haule kwa akishirikiana na wenzake Yohana Jenken Pili na Kilian
Kilian kati june 2011 na 2012 walitoa rushwa na kuwasainisha vocha za pembejeo
wananchi zaidi ya 13 wa kijiji cha Kipangala kwa malipo ya shilingi 20,000
(shilingi ishirini elfu) kila mmoja bila kuwapa pembejeo.
Mwendesha mashtaka akaongeza
kuwa makosa yote yanaangukia chini ya kifungu 15(ii)(b) cha sheria ya kuzuia na
kupambana na rushwa no 11 ya mwaka 2007, hata hivyo washtakiwa wote walikana
kuhusika na makosa yanayowakabili hata hivyo upelelezi wa kesi hizo umekamilika.
Akitoa masharti ya
dhamana hakimu Lukuna akasema dhamana iko wazi kwa washtakiwa na kwamba kila
mmoja atatakiwa kudhaminiwa na mdhamini mmoja kwa thamani ya jumla ya shilingi
1milioni kilka mmoja au mali isiyohamishika.
Washtakiwa wote
walitimiza masharti ya dhamana na kesi kuahirishwa hadi novemba 21 mwaka huu
kesi itakapokuja kwa kusikilizwa kwani upelelezi wa shsuri ulikwisha kamilika.
Katika kesi nyingine
ya udanganyifu katika pembejeo mahakama ya hakimu mkazi wilayani Ludewa
imemwachia huru Afisa mtendaji wa kijiji cha Mdilidili kata ya Lugarawa Bw
Kayombo Komnfoti na wenzake baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha
makosa yanayowakabili.
mwisho
No comments:
Post a Comment