Wednesday, September 18, 2013

NJOCOBA YAANZA KUTOA HUDUMA LUDEWA,WANANCHI WATAKA ATM HARAKA.




Na Bazil Makungu Ludewa

WANANCHI Wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe wamepongeza hatua ya uongozi wa Benki ya Wananchi njombe (NJOCOBA) kuanza kutoa huduma za kibenki mjini Ludewa na kuuutaka uongozi wa benki hiyo kuharakisha huduma ya ATM ili kurahisisha kero ya wateja kwenda kuchukua fedha ndani ya jengo hasa muda ambao benki inakuwa imefungwa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao walisema ujio wa benki hiyo ni ukombozi kwao kwani katika kipindi chote cha miaka hamsini ya uhuru Ludewa imekuwa ikitegemea benki moja tu ya NMB jambo ambalo limekuwa na usumbufu mkubwa.

Meneja wa benki hiyo tawi la Ludewa Felix Kapinga alisema tawi lake lilianzishwa julai mwaka huu na kwamba amekuwa akipokea wateja kila kunapokucha na hii nikutokana na benki yake kujali sana wananchi lakini kubwa likiwa kuwashirikisha kumiliki benki kwa njia ya kununua hisa.

‘’’’ tunazo akaunti za aina mbalimbali ikiwemo akaunti za watu binafsi, akaunti za watoto,akaunti za pamoja, akaunti za saccos, akaunti za wafanyabiashara,akaunti za makampuni na akaunti za muda maalum.’’’ aliongeza kapinga

Nani mwenye sifa ya kununua hisa za Njocoba? ni mtu yeyote wa umri wowote, kwa makampuni, asasi, taasisi, misikiti, makanisa, vijiji, serikali na vikundi dhamira ikiwa nikutumia rasrimali zilizopo kwa ajili ya kuinua hali za maisha kwa wananchi wa kima cha chini, wafanyabiashara wadogo na wa kati, wafanyakazi, wafugaji na wakulima kwa kutoa huduma bora za kifedha zinazoendana na mazingira yao.

Kapinga alizitaja faida za kununua hisa kuwa ni pamoja na kupata gawio la faida kila mwaka benki inapotengeneza faida, kuwa mmoja wa wamiliki wa benki, kushiriki mkutano mkuu wa wanahisa kila mwaka na kutoa mchango wa mawazo kwa ajili ya maendeleo ya benki, kupata faida itokanayo na ongezeko la thamani ya hisa na kutumia hisa kama dhamana ya mikopo.

mwisho

No comments:

Post a Comment