Saturday, November 16, 2013

MAAFISA WATENDAJI KORTINI KWA KUHUJUMU UCHUMI .Wasomewa mashtaka 294, wakosa dhamana na kuswekwa Lumande




                                Na Bazil Makungu Ludewa

WAKATI Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ikijipanga kuhakikisha wakulima kote nchini wanapata pembejeo kwa wakati muafaka na kuondoa ukilitimba uliojitokeza katika ugawaji wa vocha za pembejeo katika msimu wa kilimo wa mwaka jana maafisa watendaji wawili pamoja na wakala wamefikishwa mahakamani kwa makosa ya kuhujumu uchumi.

Maafisa watendaji waliofikishwa katika mahakama ya wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe ni pamoja na Ayoub Gowele afisa mtendaji kijiji cha Liugai katika kata ya Luilo, Isaack Haule kaimu afisa mtendaji kata ya Luilo, Lucas Hinjuson mwenyekiti wa pembejeo kijiji cha Liugai na Moses Mtewele wakala wa pembejeo wilayani Ludewa.

Akisoma hati ya mashtaka mbele ya hakimu mkazi mfawidhi katika mahakama ya wilaya ya Ludewa Fredrick Lukuna mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Imani Nitume aliiambia mahakama hiyo kuwa washtakiwa walitenda makosa hayo katika msimu wa kilimo wa mwaka 2010/2011 na mwaka 2013.

Nitume  aliiambia mahakama kuwa washtakiwa waligugushi lisiti za vocha za pembejeo kwa kuwadangaya wananchi 294 wa kijiji cha Liugai kusaini vocha kama walipokea vocha za pembejeo kwa manufaa binafsi huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria chini ya kifungu 333/335(d)(i) na kifungu 337 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa kanuni namba 16 kama ilivyopitiwa mwaka 2012. 

Aidha Nitume aliongeza kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na makosa mengine yakiwemo ya kula njama chini ya kifungu cha 32 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 na kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri kinyume na kifungu cha 22 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

Mengine ni ubadhirifu, uchapuzi, kugushi vocha 150 zikiwepo vocha 50 za mbolea aina ya DAP, UREA vocha 50 na vocha za mbegu 50 na kuisababishia serikali  hasara ya shilingi milioni 3.3 huku wakujua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Mshtakiwa namba tatu katika hati ya mashtaka Lucas Hinjuson alisomewa mashtaka yote bila yeye mwenyewe kuwepo mahakamani, hata hivyo washtakiwa wote walikana kuhusika na makosa hayo na kupelekwa mahabusu hadi novemba 26 mwezi huu pale mahakama itakapokuwa imepitia na kujiridhisha juu ya masharti

No comments:

Post a Comment