Monday, May 12, 2014

WAKANDARASI WAONYWA BARABARA YA LUDEWA




Na Bazil Makungu

MBUNGE wa Ludewa katika Mkoa wa Njombe Deo Filikunjombe amewaonya na kuwataka makandarasi wazarendo waliopewa na kusaini mkataba wa kazi ya kukarabati na kupanua barabara ya Itoni hadi Ludewa kuwa waaminifu na waadilifu vinginevyo hatasita kuomba mwongozo wa spika kwa yeyote atakayekwenda kinyume na mkataba.

Filikunjombe alitoa onyo hilo jana katika hafla fupi ya utiaji saini mkataba wa ukarabati na upanuzi wa barabara kwa kiwango cha changarawe kutoka itoni hadi Ludewa katika migodi ya madini ya makaa ya mawe ya mchuchuma na chuma cha Liganga ili kuwezesha kupita mitambo mikubwa.

No comments:

Post a Comment