Friday, January 30, 2015

POLISI WAUA


POLISI AUA RAIA KWA SMG ALITOROKA LINDO BENKI
. Wananchi wagoma kuuzika mwili hadi kamati ya ulinzi na usalama ifike
.Mgogoro mkubwa na visa vyatawala kati ya polisi na raia
. Dc awaomba radhi wananchi na kuwataka wapunguze jazba sheria itafanyakazi

Na Bazil Makungu Ludewa

ASKARI mwenye namba G 6352 Police constable Abduel wa kituo cha polisi Ludewa katika mkoa wa Njombe, january 23 mwaka huu majira ya saa saba za usiku alimpiga risasi kifuani na kufariki dunia hapohapo kijana ajulikanaye kwa jina la Januari Mtitu 20 fundi magari mkazi wa mtaa wa mdonga mjini Ludewa.

Akizungmza katika eneo la tukio mkuu wa wilaya ya Ludewa ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilayani hapa Juma Madaha alidhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa tayari askari anayetuhumiwa kuhusika na tukio hilo ameshakamatwa na raia wengine wawili kwa uchunguzi ili kujua chanzo cha tukio hilo.

Madaha aliwataka wananchi kupunguza jazba kufuatia tukio hilo na kwamba wasiwazuru askari wenzake kwa sababu siyo wote waliohusika kutenda kosa hili. Madaha alitoa kauli hiyo kufuatia mafundi kugoma kutengeneza jeneza na kutaka kuandamana huku wakitaka jeshi la polisi kutengeneza wenyewe ama kulipa fedha kwanza ndipo watengeneze.

’’’ tumechoka kuteswa kunyanyaswa na polisi sababu wao wanaacha kukamata wahalifu sasa wanawageukia wananchi wasio na hatia kwa kuwakamata na kuwatoza fedha bila huruma na leo wameamua kumuua mwenzetu tunataka kujua hatma ya askari huyo haraka.’’’’’ walisikika wakimweleza mkuu wa wilaya.

Imani d/o Mtitu mdogo wa marehemu yeye anasema kabla ya kakake kupigwa risasi alisikia akiongea na mtu kwa njia ya simu huku wakijibizana kwa ukali na baada ya muda walifika watu wakagonga mlango wa marehemu na alipokataa kufungua walivunja mlango na muda mfupi ulisikika mlio wa bunduki. ‘’’’ nilipotaka kutoka nje kumsaidia kakangu mlango ulikuwa umefungwa kwa nje’’’ alisema kwa masikitiko shuhuda huyo

‘’’’ nilipotaka kutoka ili kumpa msaada kaka yangu niligundua kuwa mlango umefungwa kwa nje na nilipofanikiwa kutoka nilikuta marehemu akiwa amelala chini damu zinatoka lakini anashindwa kuongea.’’’’ alisema Imani

Naye mkuu wa polisi wilaya ya Ludewa mrakibu mwandamizi wa polisi Gali ya Moshi akizungumza na gazeti hili alisema chanzo cha tukio askari Abduel Nyuki akiwa kazini kulinda benki ya NMB tawi la Ludewa alipigiwa simu na mpangaji mwenzake kwamba katika chumba chake kulikuwa kunafanyika wizi ndipo askari huyo aliacha lindo majira ya saa saba usiku na kumfuata marehemu nyumbani kwake baada ya kuambiwa na rafiki zake kuwa ndiye aliye husika.

‘’’’ pamoja na askari Abduel wapo raia wawili Juma Mhagama na Rashidi Hamadi ambao ndiyo waliomtaja marehemu kuwa mwizi na walimpeleka askari nyumbani kwa marehemu na walikuwepo wakati tukio hilo likitendeka. ‘’’ alieleza Gari ya moshi

Habari za kipolisi zinasema kuwa marehemu January Mtitu alikutwa na vielelezo kadhaa mfukoni mwake ikiwa ni pamoja na Flashi na Remote ya Tv vitu ambavyo vilitambuliwa na mshitakiwa aliyemuua marehemu askari no G 6352 pc Abduel Nyuki kuwa ni mali yake.

Taarifa za kipolisi zinaendelea kudai kuwa mbali na vielelezo hivyo kofia ya mzazi wa marehemu (pama) ilikutwa nyumbani kwa askari huyo na inadaiwa kuwa tangu mchana marehemu alikuwa ameivaa kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa wa marehemu kuiangusha wakati akitekeleza wizi huo. Hata hivyo tv ya askari ilikutwa imefichwa kwenye pagale na nyumba mbovu

Hata hivyo wakati askari wakimtuhumu marehemu kuwa alikuwa mwizi wananchi wamepinga vikali taarifa hiyo na kuongeza kuwa January Mtitu hakuwa na tabia ya udokozi hata kidogo hivyo ameonewa na kuongeza kuwa mauaji hayo yalipangwa na polisi kutokana na kuhofu kuwa marehemu angetoa siri ya wizi wa gia box ya gari la polisi PT 0764 IR 00011 Landrover mbovu.

‘’’’ askari wa kituo cha polisi Ludewa mjini walikuja kuchukua mafundi wawili ambao ni Bruno fundi pikipiki na Yohana Mtitu ili kuwasaidia kufungua gia box ya gari ya polisi na haikujulikana kama kifaa hicho kilikuwa kinapelekwa wapi ingawa baadaye habari zisizothibitika zilisikika kuwa kifaa hicho kilizua kesi ndani ya jeshi polisi mkoa.’’’’’ walisema wakazi wa Ludewa ambao hawakupenda majina yao yaandikwe

Hata hivyo polisi walikiri kufunguliwa kwa kifaa hicho kwa njia ya utaratibu wa kawaida wa kipolisi na siyo kwa njia ya wizi na kwamba gia box hiyo imefungwa katika gari la polisi lililopo katika kituo cha polisi Makambako na kwamba marehemu hakuwa mmoja kati ya mafundi waliofika kufungua kifaa hicho kwa hiyo hakuna mahusiano yoyote ya chuki kati ya polisi na marehemu.

Bruno Paulo fundi magari anasema mwaka jana dereva wa polisi aitwaye Steven alikuja gereji kwetu na kutuomba mimi na Yohane Mtitu twende kumsaidia kufungua gia box na vifaa vingine katika Landrover PT 0764 na tulipomaliza tulilipwa shilingi 20,000 na vifaa hivyo viliwekwa ktk gari ya polisi na kupelekwa Njombe ambako baada ya muda nilisikia vikamatwa na dereva wa polisi kuwekwa mahabusu.

‘’’ Siku hiyohiyo amri kutoka polisi mkoa njombe ilitolewa tu kamatwa na askari hadi kituoni ambapo tulikaa mahabusu kuanzia muda wa saa tano asubuhi hadi saa kumi na moja jiaoni ambapo tulitolewa kwa amri ya mkuu wa wilaya ya Ludewa baada ya kuwataka askari waeleze sababu ya kutuweka mahabusu wakati wao ndio waliruhusu kufunguliwa vifaa vya gari. Alieleza Bruno

Marehemu alizikwa katika makaburi ya Lugarawa mbele ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya baada ya mvutano mkali uliokuwepa kati ya wananchi wa kijiji cha Lugarawa wazazi na jeshi la polisi ambao walikuwa wakituhumiwa kumuua kwa makusudi marehemu January Mtitu.

Polisi wilayani Ludewa wamekuwa wakipewa lawama kwa kutokuwa makini na wawazi katika utendaji wao wa kazi kiasi cha kuzua lawama zisizo za msingi matukio yaliyozua tafrani na kuleta sintofahamu ni pamoja na kesi ya mbwa kumla hadi kumuua mtoto Ibrahimu chipungahelo ambaye hadi sasa haijulikani hatma ya kesi hiyo.

mwisho




































 Fulgence Ngonyani kamanda wa polisi mkoa wa njombe

No comments:

Post a Comment