Thursday, October 25, 2012

CAF YATANGAZA MAKUNDI YA AFCON 2013



WALE WABABE wa Cameroun, Kisiwa kidogo cha Cape Verde, ambao wanacheza Fainali yao ya kwanza kabisa ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2013, wamepangwa Kundi moja na Wenyeji Afrika Kusini katika Droo iliyofanyika jana na wao ndio watafungua dimba Mashindano hayo kwa Mechi rasmi ya ufunguzi dhidi ya Afrika Kusini hapo Januari 19, 2013, ndani ya Soccer City, Soweto, Johannesburg.

Mabingwa watetezi Zambia wamepangwa Kundi moja na Timu ngumu Nigeria katika Kundi C pamoja na Ethiopia na Burkina Faso.

Vigogo wengine Ghana wamepangwa pamoja na Congo DR, Niger na Mali katika Kundi B.

MAKUNDI:

KUNDI A: South Africa, Cape Verde, Morocco, Angola

KUNDI B: Ghana, DR Congo, Niger, Mali

KUNDI C: Zambia, Ethiopia, Nigeria, Burkina Faso

KUNDI D: Ivory Coast, Togo, Tunisia, Algeria


MABINGWA AFRIKA:

2012: Zambia

2010: Egypt

2008: Egypt

2006: Egypt

2004: Tunisia

2002: Cameroon

2000: Cameroon


AFCON 2013 itachezwa Afrika Kusini kuanzia Januari 19 hadi Februari 10 kwenye Viwanja ambavyo vilitumika kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2010 zilizochezwa Nchini humo.

Viwanja hivyo ni pamoja na FNB cha Mjini Johannesburg, Moses Mabhida huko Durban, Mbombela ya Nelspruit, Nelson Mandela Bay ya Port Elizabeth naRoyal Bafokeng ya Rustenburg.


No comments:

Post a Comment