Saturday, November 16, 2013

DC LUDEWA ATAKA KILA TARAFA KUWA NA SEKONDARI YA KIDATO CHA TANO NA SITA





                    Na Bazil Makungu Ludewa

MKUU wa wilaya ya Ludewa Juma Madaha amewata Madiwani katika halmashauri hiyo kuanza mpango wa kuhakikisha kila tarafa inakuwa na shule ya sekondari moja yenye yenye kidato cha tano na sita na majengo kwa ajili ya maabara za phizikia,kemia na baolojia.

Agizo hilo alilitoa jana katika ufunguzi wa kikao cha kawaida cha baraza kuu la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo alipoalikwa kama mgeni rasmi ambapo pamoja na mambo mengine Madaha aliwataka madiwani na watendaji kusimamia vizuri miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Mkuu wa wilaya ya Ludewa amefikia hatua hiyo ya kuhakikisha kila tarafa inakuwa na sekondari ya kidato cha tano na sita kutokana na wilaya yake kuwa na sekondari moja tu ya Ulayasi iliyopo katika kata ya Mlangali yenye kidato cha tano nasita kati ya sekondari 22 zilizopo katika wilaya hiyo.

Aidha Madaha amekemea vikali tabia ya wananchi wilayani Ludewa kuacha mifugo ikizagaa

No comments:

Post a Comment