Na Bazil
Makungu Ludewa
WANANCHI Wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe
pamoja na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe wamekaa kwa muda wa siku
mbili mfululizo bila kuoga ili maji
yaliyopo ili yatoshe kumhudumia rais
Dr Jakaya Kikwete na msafara wake kutokana na mji wa Ludewa kukabiliwa
na uhaba wa maji kwa muda mrefu sasa.
Akitoa taarifa mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe alimwambia
rais kuwa yeye na wananchi wanaoishi katika makao makuu ya wilaya ya Ludewa
wamekaa siku mbili mfululizo bila kuoga ili kupisha wageni walioongozana na rais wapate maji bila kubughudhiwa hii ni
kwa mujibu wa mila na desturi la kabila wa wapangwa.
Mji wa Ludewa unakabiliwa na uhaba wa maji
kwa muda mrefu sasa ambapo wananchi hao wanalazimika kutumia maji yasiyosalama
kutoka katika mto Lingalangala na chemichemi za
bonde la kigaye ambapo akina mama hulazimika kuamka usiku wa manane
kupanga foleni kusubiria maji hayo.
‘’’’ mheshimiwa Rais mimi sijaoga siku
mbili na hata wananchi waliopo hapa hawajagusa maji ili rais wao upate maji
yakukutosha, tunayo mito na maji kule milimani lakini hakuna maji tunaomba
kauli yako ya uhakika.’’’’ alisema Filikunjombe
Kwa upande wake naibu waziri wa maji Dr
Binilithi Mahenge aliwahakikishia wananchi wa Ludewa kuwa serikali imejipanga
kukabiliana na uhaba wa maji mjini ambapo alisema jumla ya shilingi b. 2.4
zimetengwa katika bajeti ya mwaka 2013/14 kwa ajili ya Ludewa.
Mahenge aliongeza kuwa jumla ya shiling
m.74 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu chakavu katika mji wa
Ludewa na kutaja chanzo kingine cha maji cha Mapetu kuwa kimetengewa jumla ya
shilingi m.300 ambapo mtego huo utakuwa km 5 na kutoa lita 345 kwa siku.
Hata hivyo waziri Mahenge alimtupia lawama
mkurugenzi wa halmashauri wa wilaya ya Ludewa na mhandisi wa maji wilaya wilaya
hiyo kutokana na uzembe wao wa kutofika Arusha kupata maelekezo na kutangaza
tenda za miradi ya maji.
Rais Kikwete anamalizia ziara yake katika
wilaya ya Ludewa ingawa ni ukamilishaji wa ziara yake katika mkoa wa Njombe leo
ambapo kesho atakuwa na mkutano wa majumuisho baada ya kuzindua mkoa huo.
mwisho
No comments:
Post a Comment