ELOY SIGARA MWEZESHAJI KUTOKA TAASISI YA CHAKULA NA LISHE DAR ES SALAAM AKITOA SEMINA KWA MAAFISA AFYA WILAYA YA LUDEWA NA WADAU WA CHUMVI
VUMILIA LYATUU KUTOKA TAASISI YA CHAKULA NA LISHE TAIFA AKITOA MADA KWA WASHIRIKI WA SEMINA YA MATUMIZI YA CHUMVI YENYE MADINI JOTO YA KUTOSHA
AFISA AFYA WILAYA YA LUDEWA KELVIN MFUSE WA KWANZA KULIA NA MWENZAKE WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA SEMINA HIYO
WAFANYABIASHARA YA CHUMVI WAKIPATA SEMINA KUHUSA UTUNZAJI WA CHUMVI KABLA HAIJAFIKA KWA MLAJI
CASTORI KIBASSA AFISA AFYA AKIONESHA KWA WASHIRIKI KIFAA CHA KUPIMIA CHUMVI
CHUMA CHA LIGANGA
KIJIJI CHA AMANI AMBACHO KIPO KATIKA ORODHA YA VIJIJI VINAVYOTARAJIA KUHAMA KUPISHA MGODI
SAMAKI WA ZIWA NYASA AINA YA MBUFU WAKIWA SOKONI SAMAKI MMOJA ANAUZWA KWA YA SHILINGI 5000
WANANCHI WENGI NCHINI HAWANA ELIMU YA KUTOSHA KUHUSU MATUMIZI YA CHUMVI YENYE MADINI JOTO YA KUTOSHA
WANANCHI wametakiwa kukabiliana na
magonjwa yanayotokana na upungufu wa madini joto mwilini kwa kudai na kununua
chumvi yenye madini joto ya kutosha ili kukabili tatizo hilo linaloathiri afya
na maendeleo ya jamii pamoja na kushuka kwa uzalishaji mali na uchumi.
Takwimu hizo zilitolewa jana na taasisi ya
chakula na lishe nchini kwenye semina ya siku moja kwa wadau mbalimbali
iliyofanyika wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe ambapo ilionesha kuwa madini
hayo huagizwa nje ya nchi kutokana na Tanzania kukosa kabisa madini hayo
muhimu.
Akizungumza katika semina hiyo Eloy Sigara
mwezeshaji kutoka taasisi ya chakula na lishe Tanzania alisema kutokana na
madini joto kuagizwa ndiyo maana kilogram moja nchini huuzwa kwa shilingi
95,000 jambo linalopelekea watengenezaji wa bidhaa hiyo muhimu kushindwa kumudu
bei na kuamua kutengeneza na kuuza chumvi isiyo na madini joto ya kutosha.
‘’’’’ tatizo la upungufu wa madini joto
hapa Tanzania ni la tatu kwa ukubwa katika matatizo ya lishe likitanguliwa na
tatizo la nishati na upungufu wa akili na mkoa wa njombe unakabiliwa na tatizo
kubwa hivyo kila kaya inatakiwa kupata chumvi yenye madini joto ya kutosha’’’’
alisema Sigala
Naye bi Vumilia Lyatuu kwa upande wake
akawataka washiriki wa semina hiyo hasa maafisa wa afya wilaya, kata na vijiji
kutoa elimu kwa wananchi juu ya athari zinazotokana na ukosefu wa wa madini
hayo hususani akina mama wajawazito kuwa ni pamoja na mimba kuharibika, mtoto
kuzaliwa kabla ya muda wake au kuzaliwa mfu, kuzaliwa na mtindio wa ubongo na
kuchelewa kubarehe, udumavu wa ubongo na mwili,kuzaliwa na ulemavu wa viungo na kadharika.
Lyatuu alisema utafiti wa awali
uliofanyika mwaka 1980 takwimu zilionesha kuwa asilimia 40 ya watanzania
walikiri kuishi kwenye maeneo yenye upungufu wa madini joto ambapo asilimia 25
ya watanzania walikuwa wameathirika na
uvimbe wa tezi la shingo(goitre).
Aliitaja mikakati ya serikali kuwa ni
pamoja na kuagiza mashine na vifaa vya kuchanganya chumvi na madini joto,
utoaji wa madini joto ya nyongeza na vidonge vyenye madini joto, kutoa elimu
kwa makundi mbalimbali kwa kutumia njia ya radio, magazeti na television,
kuanzishwa kwa sheria ya chumvi,kuwaunganisha wazalishaji chumvi na wadau
wengine nchini.
Mikakati mingine ni kuweka mfumo wa
ufuatiliaji, kuwepo na kamati ya kitaifa inayoratibu mpango wa kudhibiti upungufu
wa madini joto kwa kuwa na wajumbe kutoka wizara mbalimbali ikiwemo wizara ya
afya, madini,fedha, na viwanda na biashara.
Hata hivyo changamoto zinazoikabili
taasisi ya chakula na lishe ni pamoja na
wazalishaji kutofuata vigezo vya uzalishaji bora wa chumvi yenye madini joto,
viwango vya madini joto, usafi na uhifadhi, uwepo wa wazalishaji wadogo wengi
wa chumvi waliotawanyika katika maeneo tofauti, kutokuwepo na upatikanaji
endelevu wa madini joto na mapungufu katika mfumo wa usambazaji.
Ni kutokana na changamoto hizo maafisa
afya katika ngazi za wilaya, kata na vijiji wilayani Ludewa walipitisha
maazimio katika maeneo yao na kuhakikisha jamii inatumia chumvi yenye madini
joto ya kutosha, kutoa elimu kwa umma juu ya matumizi ya chumvi yenye madini
joto, kuhamasisha jamii juu ya utunzaji chumvi, sheria ya chumvi, kuingiza
haraka kwenye kamati za maendeleo za kata, kupima ubora wa chumvi katika ngazi
ya kaya na suala la chumvi yenye madini kuwa suala la mtambuka na kuwasilisha
taarifa ya utekelezaji kila baada ya robo mwaka.
mwisho






.jpg)






No comments:
Post a Comment