Monday, March 24, 2014

FILIKUNJOMBE AENDESHA HARAMBEE YA UNUNUZI WA GARI LA PAROKIA WANANCHI WASEMA NI NURU YA KWELI. Milioni 30.7 kati ya m. 90 zapatikana papohapo




              Na Bazi Makungu Ludewa
MBUNGE wa jimbo la Ludewa katika Mkoa wa Njombe Deo Filikunjombe amefanikiwa kuchangisha papohapo jumla ya shilingi m.30.7 kati ya shilingi m.90 zinazotakiwa na kusakwa na waumini wa kanisa katoliki kwa ajili ya ununuzi wa gari la parokia ya Ludewa mjini.

Harambee hiyo ilifanyika machi mwaka huu katika kanisa la yesu kristu mkombozi lililopo Ludewa mjini ambapo ilifanyika misa maalumu kwa kuwashirikisha waumini kutoka vigango vyote vinyounda parokia hiyo ambavyo ni pamoja na Nyamapinda, Ludewa(K) na Ngalawale.

Ujio wa mbunge huyo ulikuja kufuatia mwaliko wa kamati ya ununuzi wa gari ambayo ilimtuma diwani wa kata ya Ludewa Monica Mchiro na mwenyekiti wa kamati hiyo mzee Kayombo kumwomba Filikunjombe kuja kuendesha harambee hiyo.
 




No comments:

Post a Comment