Thursday, May 8, 2014


AFISA MTENDAJI ATAFUNA PESA YA MRADI WA MAJI
.ashindwa kulipa nyumba yake yapigwa mnada na balaza la kata

Na Charles Mhagama Ugela Mkongobaki

AFISA mtendaji wa kijiji cha Ugela kata ya mkongobaki tarafa ya Liganga Ludewa katika Mkoa wa Njombe Xavery Haule amalazimika kuiacha nyumba na kujisitili kwa majirani baada ya balaza la kata kuiuza nyumba yake kutokana na kesi ya kutafuna bila huruma jumla ya shilingi 230,000 za mradi wa maji katika kijiji hicho.

Tukio la kuuzwa kwa nyumba ya mtumishi huyo wa umma lilifanywa na balaza la kata ya Mkongobaki Aprili 23 mwaka huu baada ya mshtakiwa kushindwa kulipa pesa hiyo ya kijiji kwa awamu kama alivyoahidi alipokabidhi nyumba kama dhamana yake.

Akizungumza na gazeti hili John Mhagama ambaye ni karani wa balaza hilo alikiri kuwepo kwa kesi hiyo na kuongeza kuwa balaza limelazimika kuuza nyumba ya Bw Xavery Haule baada ya kushindwa kutekeleza ahadi yake ya kulipa pesa kwa awamu kama alivyoomba.

‘’’’’’ wananchi wa kijiji cha ugela walibuni mradi wa maji na kuamua kuchanga kila kaya na zikapatikana jumla ya shilingi 230,000 kwa ajili ya kujenga tanki la maji lakini afisa huyo akaziweka mfukoni na alipoitwa kwenye kamati ya maendeleo la kata (KAMAKA) alikiri na kuamuriwa kulipa polepole kwa awamu aliposhindwa kulipa kesi ilipelekwa balaza la kata.’’’ alisema mhagama

Kwa upande wake afisa mtendaji Exavery Haule alipoulizwa na gazeti hili kuhusu tuhuma na hukumu aliyopata alikiri kukusanya fedha 230,000 kwa ajili ya mradi wa maji kutoka kwa wenyeviti wa vitongoji vya Kigina na Mlangali ndani na kuongeza kuwa hakustahili kupewa hukumu hiyo kwa sababu fedha ilifanya kazi halali na mwenyekiti anatambua.

‘’’’’ nimesikitishwa na hukumu iliyotolewa na balaza la kata kwa sababu pesa hiyo sikutumia kwa manufaa yangu bali zilitumika kwa shughuli halali ya kupokea wageni na wafadhili toka Hispania waliofika kuangalia mradi wa maji na nilikubaliana na mwenyekiti.’’’’ alisema Xavery

Akifafanua matumizi ya fedha hiyo Haule sh105,000 zilitumika kununua kuku 6 kama kitoweo cha wageni, sh12,000 mchele kg 5, sh45,000 soda creti 3, sh10,000 ulanzi lita 40, sh16,000 pombe lita 40, sh14,400 maji ya kunywa, sh15,000 nyama kg 2 na viungo, sh5000 debe la viazi, sh 8000 mafuta ya kupilia, sh 9000 vikapu kwa ajili ya zawadi ya wageni.

Vingine ni sh 6000 nyungo kwa ajili ya zawadi ya wageni, sh2,600 viungo na mboga za majani, sh5000 vocha, 5000 alimpa mwenyekiti wa kijiji.

MWISHO


No comments:

Post a Comment