WATANZANIA WAMETAKIWA KUANDIKA VIJALIDA
ILI KUTUNZA KUMBUKUMBU NA KUSOMA VITABU ILI KWENDA NA WAKATI.
. Asema ukitaka kumnyima mtanzania pesa
weka ndani ya kitabu.
Na Bazil Makungu
ASKOFU
Mstaafu wa kanisa la kiinjili la kilutheri Doyasisi ya kusini kati
Wilayani Makete katika Mkoa wa Njombe dakta Solomon Swallo amewataka
watanzania kujenga utamaduni wa kusoma na kuandika vitabu katika
maisha yao ya kila siku ili kujitunzia kumbukumbu na kupanua uelewa
katika mambo mbalimbali.
Askofu
Swallo aliyasema hayo hivi karibuni katika kanisa hilo usharika wa
Bulongwa alipotunukiwa shahada ya uzamivu (PHD) na chuo cha nchini
marekani ambapo pamoja na mambo mengine alikuwa akisherekea miaka
themanini na moja(81) tangu kuzaliwa kwake.
Askofu
Swalo aliyelitukia kanisa kwa miaka 24 akiwa askofu wa doyasisi ya
kusini alionesha kusikitishwa kwake na tabia ya watanzania wengi
kupenda mambo ya starehe na burudani mbalimbali huku wakiweka pembeni
suala muhimu la uandishi na usomaji wa vitabu.
“”” ndugu
zangu watanzania ninyi ni watu wa ajabu sana nashangaa kuona watu
wanaweza kukaa wiki nzima hata mwezi hajasoma kitabu chochote,
ukitaka kumnyima pesa mtanzania weka katika kitabu utazikuta zikiwa
salama kwa sababu hawana utamaduni wa kusoma vitabu.”””
alionesha maskitiko askofu Swallo
Kutokana
na uvivu huo Swallo amewataka watanzania wote kujizoeza kuandika
masuala ya kawaida na kutunza kumbukumbu hata katika vijarida vyenye
kurasa chache zenye kuelezea matukio mbalimbali yakiwemo mambo
yanayotokea kila siku katika jamii zao bila kusubiri matukio makubwa.
mwisho
No comments:
Post a Comment