Thursday, May 8, 2014


MAFURIKO MTO LUHUHU YAHARIBU MAZAO HEKTA 126 ZA MPUNGA ZAMEZWA NA MAJI.

Na George Ngalawa Manda

WANANCHI wanaoishi kwenye vijiji vilivyopo kata za Luhuhu na Manda katika tarafa ya Masasi wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe wamo hatarini kukosa chakula mwaka huu kutokana na mto Luhuhu kujaa maji kufuatia mvua kubwa inayoendelea na kudumu zaidi ya mwezi sasa.

Wakulima walioathirika na mafuriko hayo ni pamoja na wale wanaolima mashamba ya mihogo na mpunga katika vijiji vya Ngelenge, Kipingu, Ilela, Nsungu na Fokland ambao sasa wamelazimika kuhama makazi yao kutokana na maji kujaa katika nyumba zao.

Afisa kilimo na mifugo Faraja Mpunga akitoa takwimu alisema kufuatia mafuriko hayo hekta 126 za mpunga zimemezwa na maji, hekta 29 za mihogo na mahindi hekta 28.25 na kuongeza kuwa mafuriko hayo yanatokana na mvua kubwa iliyonyesha machi 31 mwaka huu.

Akizungumza na radio uplands afisa mtendaji wa kata ya Luhuhu Musa Kazimoto alisema mafuriko hayo yalianza machi 31 mwaka huu katika mashamba ya wananchi ambapo tangu wakati huo mpaka sasa mazao yamefunukwa na maji.

Kazimoto alisema kufuatia mafuriko hayo ofisi yake imetoa taarifa katika ngazi vikiwemo vyombo vya serikali lakini wamekuwa wakifiki na kuondoka kufuatia hali hiyo serikali za vijiji zimetoa maelekezo kwa wananchi ili waanza kuondoa mazao ambayo yanaweza kuokolewa kwa kutumia mitumbwi.



                   mwisho


WATUMISHI WAMLAUMU MKURUGENZI WAO MEI MOSI.
.Sherehe ilipelekwa kijijini kwao lakini zawadi zikarudi mjini

Na Enhard Mwachiro Lugarawa

WATUMISHI na wafanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa katika mkoa wa Njombe waliopo vijijini wamemlalamikia mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo kwa kutokutenda haki katika utoaji zawadi kwa wafanyakazi bora katika sherehe za mei mosi mwaka huu.

Hayo yamesemwa na wafanyakazi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi (mei mosi) iliyofanyika kiwilaya katika kijiji cha Lugarawa tarafa ya Liganga ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya ya Ludewa Juma Madaha.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wafanyakazi hao walisema sherehe hizi kiwilaya zimefanyika kama maigizo kwamba pamoja na changamoto walizonazo za kufanyakazi katika mazingira magumu wanakatishwa tamaa na mwajiri wao kutokana na kutoa zawadi na wafanyakazi bora kwa upendeleo.

‘’’’’ zaidi ya asilimia 80 ya wafanyakazi waliopata zawadi za ufanyakazi bora mwaka huu walitoka nao mjini kuja kufanya maigizo huku Lugarawa lakini mbaya zaidi wengine tumeshuhudia wakipata zawadi hizo kila mwaka kuna nini? Aliuza mwalimu mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe

Wamesema hakuna sababu ya kupeleka sherehe za mei mosi katika maeneo ya vijijini wakati wanaonufaika ni wafanyakazi wa mjini. ‘’’’’ tunamwomba mkurugenzi aache kutudhihaki kama siku nyingine afanye sherehe hizo karibu na watu wake anaopendelea kuwapa zawadi za ufanyakazi bora.’’’’ alilalamika muuguzi mmoja

Aidha katika risala yao kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Ludewa wafanyakazi katika halmashauri hiyo wametaja shinikizo la damu kama chanzo cha vifo kwa watumishi wengi wilayani humo.

Akisoma risala ya wafanyakazi mbele ya mgeni rasmi katibu mkuu wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi wilaya ya Ludewa Joseph Mvanga alisema wafanyakazi wamekuwa wakipoteza maisha kwa magonjwa mbalimbali lakini kubwa ikiwa shinikizo la damu kutokana na kudai mafao yao bila mafanikio, kutopandishwa mishahara na vyeo.

Mvanga alisema mwajiri amekuwa na kiburi na kuvaa miwani ya mbao kama vile haoni matatizo ya watumishi wake huku akiziba masikio kwa pamba kama vile hasikii kelele na kilio cha watumishi wake jambo linalopelekea wafanyakazi kufa kwa mawazo na maisha magumu.

Akijibu risala hiyo mkuu wa wilaya ya Ludewa Juma Madaha aliwaondoa hofu watumishi na wafanyakazi katika halmashauri ya wilaya kwa kuwaambia kuwa madai yao yatashughulikiwa.


            mwisho

No comments:

Post a Comment