Saturday, October 13, 2012

VURUGU ZA WAISLAMU NA JESHI LA POLISI JANA


Hii ndio hali halisi ilivyokuwa kamata piga, kamata piga, peleka kwenye gari na kisha kupelekwa kwenye vituo vya Polisi kuhifadhiwa. Wananchi hawa waliamua kukaa chini ili kusalimu amri lakini hiyo haikuwaponya baada ya kuzuka kwa vurugu kati ya waislamu na jeshi la polisi zilizoanzishwa na waislamu baada ya kudaiwa kutokea kwa mabishano ya watoto na mmoja wao kukojolea kitabu cha kuran hapo jana maeneo ya Mbagala kizuiani jijini Dar es salaam
Baadhi ya wakazi wa eneo hilo, wakizungumza na waandishi wa habari, kulalamikia mabomu na kudai kuwa yalikuwa yakiwaumiza sana kwani mchana kutwa wa leo, hali ilikuwa ni mbaya hasa ikizingatiwa watoto walikuwa wamelazwa majumbani na hivyo kuathiriwa na mabomu hayo. PICHA KWA HISANI YA BAYANABLOGSPOT


Polisi wakiwaingiza kwenye gari, vijana waliowanasa kwenye vurugu hizo.
Hawa ni baadhi ya vijana waliokamatwa kwenye vichochoro mbalimbali vya eneo hilo baada ya kukimbia mabomu na kujificha.
Asakari wa Jeshi la Polisi, Kikosi cha FFU wakiruka mtaro na watuhumiwa wavurugu zilizo zuka leo kwenye eneo la Mbagala Kizuiani baada ya mtoto anaedaiwa kuwa wa kidato cha kwanza kudaiwa kuikojolea Qurani Tukufu na kusababisha taharuki kubwa mchana wote wa leo, ambapo hadi jioni Mbagala ilikuwa bado vurugu zikiendelea.
Hapa ikawa piga nikupige tu hadi askari hao kufanikiwa baadhi ya vijana hao kuwatia nguvuni huku wakiwapa kisago cha nguvu.

No comments:

Post a Comment