Na Bazil Makungu Ludewa
MBUNGE wa jimbo la Ludewa
katika mkoa wa Njombe Deo Filikunjombe jana alilazimika kumfukuza
kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya na wakuu wa idara baada ya
kushindwa kutoa maelezo kuhusu vilipo vitanda, magodoro na mashuka
vifaa alivyovinunua yeye mwenyewe mwaka mmoja uliopita kwa ajili ya
zahanati ya Ihanga iliyopo kata ya Mlangali.
Awali Filikunjombe
alikataa kufanya mkutano katika uwanja uliokuwa umeandaliwa badala
yake akamtaka mwenyekiti wa kijiji cha mlangali ndani kuwaita
wananchi na kufungua mkutano kwenye viwanja vya zahanati hiyo
Katika ziara yake ya wiki
moja ya kukagua miradi ya maendeleo jimboni kwake Filikunjombe
alifuatana na kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Horace Kolimba
akiwemo kaimu mganga mkuu na wakuu wa idara za kilimo, maji na
ujenzi.
Hali ya hewa ilianza
kuchafuka katika mkutano baada ya Filikunjombe kukagua zahanati na
kugundua mapungufu mengi ikiwemo ukosefu wa vitanda vya kupumzikia
wagonjwa na akina mama na kitanda cha kujifungulia vifaa ambavyo
alivinunua mwenyewe na kutoa fedha ya usafiri na kuikabidhi
halmashauri ya wilaya kwa ajili ya kupeleka katika zahanati lakini
wamekaa navyo huku wananchi wakiendelea kusafiri umbali mrefu kufuata
matibabu.
Kwa upande wake kaimu
mkurugenzi Horace Kolimba baada ya kukosa majibu alimwomba
Filikunjombe ampe wiki moja ili aweze kuvifikisha vifaa hivyo lakini
kwa mbunge ilikuwa vigumu kukubali ombi hilo na ndipo hatua ya
kuwafukuza ilitimia na kusimamisha mkutano kwa muda mpaka vifaa vyao
vitakapoletwa.
‘’’ wananchi
mmejionea wenyewe wameshindwa kutoa majibu mbele yenu sasa
hatuendelei na mkutano waondoke hapa wakalete vifaa vyetu ndipo
mkutano uanze hatuwezi kukaa hapa tunapiga siasa wakati huduma za
zahanati zimekaliwa na watendaji, serikali yetu na chama cha
mapinduzi inaonekana haifanyikazi kwa sababu ya watendaji wabovu
kwenye jimbo langu siwezi kuwavumilia.’’’ alilalamika
filikunjombe
Umbali kutoka ilipo
zahanati ya Ihanga Mlangali na makao makuu ya wilaya ni takribani
kilometa 75 lakini kutokana na msimamo wa mbunge wao wananchi
walikubali kusubiri bila kuchoka huku wakitumbuiza na kucheza ngoma
za asili mpaka vifaa vyote vilipofika na kuhesabiwa na kisha
kukabidhiwa kwao.
‘’’ mafuta ya gari
la mkurugenzi na posho yake havikosekani katika halmashauri ya wilaya
ya Ludewa lakini mafuta ya kuleta vifaa katika zahanati kwa kipindi
cha mwaka mzima wanasema hayapo na sasa hivi tunavyoongea mkurugenzi
Wiliam Waziri yuko mbeya kuzifuata posho. Alisikitishwa filikunjombe
Diwani wa kata hiyo
kupitia chadema Faraja Mlelwa alimpongeza mbunge huyo kwa kuchapa
kazi na kuwatumikia wananchi kwa moyo wote bila ubaguzi na kusema
kuwa katika suala la maendelea lazima tuweke itikadi zetu pembeni na
kuahidi kutoa ushirikiano.
mwisho
No comments:
Post a Comment